• Do you have any questions?
  • T: +255 22 26 00 944 |
  • M: +255 753 912 130
  • info@wftrust.or.tz
  • WHISTLE BLOWER
  • MEDIA & PUBLICATIONS
  • WFT
  • WHO WE ARE
    • OUR HISTORY
    • OUR WORK
    • OUR TEAM
    • JOIN US
  • COALITIONS
  • GRANTS
    • APPLY FOR A GRANT
    • OUR GRANTEE PARTNERS
  • OUR BLOG
    • GALLERY
  • CONTACT US
NEW PARTNERSHIP WITH IRELAND
September 24, 2018
TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MAJIBU YA MAOMBI YA RUZUKU YA MIRADI KATIKA KUKUZA UELEWA WA HAKI ZA WANAWAKE, WASICHANA NA WATOTO TANZANIA KATIKA KIPINDI CHA KUPAMBANA NA COVID 19.
May 20, 2020

TAARIFA KWA WAOMBAJI WA RUZUKU ZA KUTEKELEZA AFUA MBALIMBALI MWAKA 2020

Awali ya yote tunapenda kuwashukuru wote mliowasilisha maombi ya ruzuku kwetu kwa mwaka 2020.Tunafurahishwa na idadi ya waombaji wa ruzuku inayoendelea kuongezeka mwaka hadi mwaka

Wapendwa washirika na waomba ruzuku.

Awali ya yote tunapenda kuwashukuru wote mliowasilisha maombi ya ruzuku kwetu kwa mwaka 2020.Tunafurahishwa na idadi ya waombaji wa ruzuku inayoendelea kuongezeka mwaka hadi mwaka.

Pili tungependa kuwajulisha kuwa WFT-Trust kama taasisi imekuwa sehemu ya kuathirika na kubainika kwa wagonjwa wa mafua makali ya CORONA kama ambavyo tumetaarifiwa na mamlaka husika tangu juzi.

Hali hii ya kuwepo kwa wagonjwa hawa nchini mwetu imetulazimisha kupitia taratibu zetu za kiusalama wa afya na taratibu zetu za utoaji huduma.

Sisi kama taasisi tumefanya tafakari ya kina kuhusu athari mtambuka za hali ya ugonjwa huu na jinsi ambavyo tunapaswa kuchukua tahadhari ili kuepusha maambukizi mapya ya ugonjwa wa CORONA kwetu sisi wenyewe lakini pia kwa wadau na washirika wetu mbalimbali maana kama tujuavyo ‘’Kinga ni Bora Kuliko Tiba”. Baada ya tafakuri ya kina tumefanya maamuzi yafuatayo ambayo yamepelekea kuwepo na mvurugizo wa taratibu zetu za kawaida za utendaji kazi na hususan utaratibu wa utoaji ruzuku.

Hatua tulizochukua:

  • Tumesitisha safari za kikazi za ndani na nje kwa wafanya kazi wetu
  • Tumesitisha mikutano,makongamano na warsha kwa vile huleta mijumuiko ya wadau wengi kwa pamoja
  • Tuna uwezekano wa kusitisha kufanya kazi tukiwa ofisini na kufanyia kazi kutoka majumbani
  • Tumesitisha baadhi ya hatua katika mchakato wa utoaji ruzuku kwa muda hasa hatua vile zinazohusisha mchakato wa kuwatembelea waombaji katika hatua za uhakiki na kujiridhisha.
  • Tunaendelea kuangalia hali ya maendeleo ya ugonjwa huu na athari zake mtambuka ili kufanya maamuzi yenye tija katika siku za usoni.

Athari za hatua hizi:

  • Kuchelewa kwa mchakato wa utoaji ruzuku ambapo tunakisia kutakuwa kati ya wiki 4 mpaka sita kuanzia tarehe ya leo 23/03/2020
  • Kucheleweshwa kwa kutoa mrejesho juu ya kupokelewa kwa maombi husika
  • Kusitishwa kwa mikutano ya kikazi hapa ofisini baina yetu na waombaji wa ruzuku kwa kipindi cha walau wiki mbili za kwanza

Hitimisho:

Pamoja na nia yetu njema ya kuharakisha michakato ya kutoa ruzuku kwa washirika wetu tunatambua changamoto mbalimbali zinazotokana na hali ya ugonjwa huu hatari na wajibu wetu wa kujali na kulinda afya na usalama wa wafanyakazi wetu,washirika wetu pamoja na wadau wetu mbalimbali.

Moja ya adhari kubwa ya hatua hizi ni kuchelewa kwa mchakato wa utoaji wa ruzuku kwa mwaka huu ambayo itaathiri pia uwezo wa wadau wetu katika kutekeleza afua mbalimbali za utetezi wa haki za binadamu na hususan hati za Wanawake,Wasichana na Watoto.

Hivyo kwa taarifa hii tunaomba mpokee salamu zetu za upendo na mshikamano kwenu nyote katika kipindi hiki kigumu.

Mwisho tunakisia kuwa michakato kwa ujumla itachelewa kwa muda wa kati ya wiki 4 mpaka 6.

Tunaomba radhi kwa uchelewesho huu na tunawaomba msikate tamaa na kwamba mara tu baada ya hali ya udhibiti wa mlipuko wa ugonjwa huu kutengemaa tutaendelea na mchakato wa utoaji wa ruzuku kama kawaida.

Tutaendelea kupatikana na kutoa huduma na au ushauri mbalimbali kwa wadau wetu kupitia mawasilano ya simu kwa nambari 0753 912130, barua pepe kwa anuani ya info@wft.or.tz na inapowezekana kupitia mikutano mkondoni (Online meetings).

Asanteni Sana

Imetolewa na Mkurugenzi Mtendaji,
Mary Rusimbi

WFT-Trust,
Dar es Salaam
23/03/2020.


Share
15
wftadmin
wftadmin

Related posts

March 15, 2022

SUPPORT FEMINIST MOVEMENTS IN UKRAINE, POLAND, and BULGARIA NOW!


Read more

Intersectionality is important in tackling inequalities and injustices towards women, girls, children and other social justice actors so as not to perpetuate inequality in systems.

March 7, 2022

STRENGTHENING THE SEXUAL AND REPRODUCTIVE HEALTH RIGHTS COALITION


Read more
June 29, 2021

THE WOMEN’S MOVEMENT CELEBRATES 100 DAYS OF HER EXCELLENCY MADAM PRESIDENT SAMIA SULUHU HASSAN IN OFFICE


Read more

About us

WFT Logo-footer grey

Women Fund Tanzania Trust is a registered Trust and the first women’s rights fund in the country both as a movement builder, and as an activist and feminist organization,

Our Mission

To contribute to the building of a strong women’s movement in Tanzania through making grants, strengthening women’s capacity, building strategic alliances and mobilizing resources.

Our Vision

To see a Tanzanian society where women realize their full potential and engage fully in the transformation of their communities in order to achieve empowerment and social justice.

Recent Posts

  • Beloved Christina M. Warioba: Sunrise September 28, 1952 – Sunset May 31, 2022
  • SUPPORT FEMINIST MOVEMENTS IN UKRAINE, POLAND, and BULGARIA NOW!
  • STRENGTHENING THE SEXUAL AND REPRODUCTIVE HEALTH RIGHTS COALITION
  • Beloved Zukivah Njalai Mihyo Sunrise September 28, 1952 – Sunset August 20, 2021
  • THE WOMEN’S MOVEMENT CELEBRATES 100 DAYS OF HER EXCELLENCY MADAM PRESIDENT SAMIA SULUHU HASSAN IN OFFICE

Contact Us

Write to us using the following address:
P. O. Box 79235 Msasani,
Dar es Salaam, Tanzania.

T: +255 22 26 00 944
M:+255 753 912 130

Write to us: info@wftrust.or.tz

Visit us:
17 Rufiji Street, Masaki,
Dar es Salaam, Tanzania.

© 2016 Women Fund Tanzania Trust. All Rights Reserved.
[contact-form-7 id="2322" title="WFT"]